Jn  JL, 2008  Agst

S M T W T F S
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031  

2007  2008  2009

 
 

Maendeleo ya Mtandao:
Kitengo cha Huduma za Mtandao za UM, Idara ya Habari kwa Umma, Hakimiliki © , Umoja wa Mataifa, 2006


??????????? ?????For download Right click and save as

A’khms 03 JL 2008 | hamishia mp3

bullet

Mkuu wa UN-HABITAT anaelezea umuhimu wa kudumisha makazi kuimarisha maendeleo
Mnamo mwanzo wa wiki Baraza la UM juu ya Maendeleo ya Uchumi na Jamii, yaani Baraza la ECOSOC, lilianzisha mijadala maalumu ya hadhi ya mawaziri, kufanya mapitio ya ripoti za Mataifa Wanachama juu ya mafanikio yaliojiri katika utekelezaji wa kitaifa, na kikanda, kwenye ile ajenda ya UM kuhusu shughuli za maendeleo. Wajumbe wa Baraza hilo walisailia kipamoja hatua za kuchukuliwa kimataifa kuondosha vizingiti vinavyokwamisha ustawi wa uchumi na jamii katika mataifa yanayoendelea.

bullet

Hapa na pale
KM Ban Ki-moon alipohutubia Chuo Kikuu cha Taifa cha Seoul, katika Jamhuri ya Korea, baada ya kupokea shahada ya hishima, alitoa mwito maalumu kwa wananchi wenzake uliowataka waongeze mchango wao kwenye juhudi za kutatua masuala magumu yanayosumbua ulimwengu wetu, mathalan, kupanda kwa kasi kwa bei za chakula, mifumko ya bei za mafuta na vile vile hatari inayopaliliwa na ugaidi.

bullet

KM amewasili Jamhuri ya Korea kwa ziara rasmi
KM Ban Ki-moonn Alkhamisi alifanyiwa mapokezi ya kishujaa alipowasili Jamhuri ya Korea (Korea ya Kusini), taifa aliozaliwa. Hii ni ziara rasmi ya awali kwa KM Ban tangu alipochukua madaraka ya kuongoza UM katika miezi 18 iliopita.

bullet

Ukombozi wa mateka 15 Colombia wapongezwa na KM
KM amepokea kwa ukunjufu mkuu taarifa ya Serikali ya Colombia kuwa imefanikiwa kuwaokoa mateka 15 walioshikwa na wanamgambo wa Jeshi la Mapinnduzi katika Colombia au FARC.

bullet

ICC imeamrisha Lubanga aachiwe, halan
Mahakama ya Kimataifa juu ya Jinai ya Halaiki (ICC) imeamrisha Thomas Lubanga Dyilo aachiwe, mtuhumiwa wa kwanza aliyekabili mashtaka kwenye Mahakama hiyo tangu ilipobuniwa. Kwa mujibu wa Mwendesha Mashtaka, Lubanga alituhumiwa kuajiri watoto wa umri mdogo waliolazimishwa kushiriki kwenye mapigano katika eneo la Ituri katika kipindi cha baina ya 2002 hadi 2003.

bullet

Bemba amehamishwa kizuizini Hague
Kadhalika Alkhamisi ya leo aliyekuwa Naibu Raisi wa JKK, Jean-Pierre Bemba amehamishwa kutoka Burussels, Ubelgiji na kupelekwa kizuizini mjini Hague, Uholanzi yalipo makao ya Mahakama ya ICC, ambapo atawekwa akisubiri kesi. Bemba ametuhumiwa kuongoza wafuasi wa kundi lake la MLC, kuendeleza vitendo haramu vya kunajisi kimabavu raia na kuwatesa watu, katika miaka ya 2002 hadi 2003 nchini JKK.

bullet

Korti ya Rufaa ya ICTY imemwachia huru Kamanda wa Bosnia
Korti ya Rufaa ya Mahakama ya Kimataifa juu ya Yugoslavia ya Zamani (ICTY) imemwachia Naser Oric, aliyekuwa kamanda wa vikosi vya Waislamu wa Bosnia katika maeneo ya Srebrenica. Alituhumiwa kuzuia wanajeshi waliokuwa chini ya uongozi wake kutoangamiza vijiji 50 vya WaSerb mnamo 1992 mpaka 1993, tukio ambalo linaripotiwa lilisababisha maelfu ya watu kuhama makwao.

bullet

Misaada ya kihali kuhudumiwa tena Abyei na UM
Hali ya utulivu imerejea katika eneo la Abyei, Sudan sasa hivi baada ya fujo zilizochipuka huko mwezi Mei. Shirika la Afya Duniani (WHO) likijumuika na mashirika mengine ya UM yameanza kuandaa miradi ya kihali kadha wa kadha ya kuwarudisha makwao maelfu ya watu waliohajiri makazi kufuatia mifumko ya vita siku za nyuma. Mashirika haya yanatarajiwa kuwapatia umma husika huduma za kihali ili kuanzisha maisha kwenye mazingira ya utulivu.

Print Today's News

A’khms 03 JL 2008

sikiliza | hamishia mp3
G-8 inatakiwa izingatie kihakika mifumko ya bei za chakula na mafuta duniani

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwenye ripoti mpya iliotolewa wiki hii, imekumbusha kwamba mfumko wa bei za chakula pamoja na muongezeko wa kasi wa bei za mafuta katika soko za kimataifa, ni vitendo vinavyoathiri sana nchi masikini na yale mataifa ya maendeleo ya wastani, nchi ambazo kikawaida hulazimika kuagizishia bidhaa hizo kutoka nje.


sikiliza | hamishia mp3
Adhabu za kifo Marekani zinatathminiwa na Mkariri Maalumu wa Haki za Binadamu

Profesa Philip Alston ni Mkariri Maalumu wa UM anayehusika na haki za binadamu zinazofungamana na masuala ya hukumu ya vifo, nje ya sheria, pamoja na mauaji ya kihorera. Majuzi Alston aliwakilisha mbele ya waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu ripoti maalumu iliosailia namna hukumu ya vifo inavyotekelezwa katika taifa la Marekani.



 

sikiliza | hamishia mp3 | archive

Tathmini ya Mradi wa Milenia, Mbola, Tanzania (Sehemu ya II)
Mileniam Bola Office
Katika makala iliopita tulikupatiani fafanuzi, za awali, za Dr. Gershon Isaac Nyadzi, mratibu wa sayansi na pia Mtafiti Mwandamizi anayeongoza timu ya wataalamu wanaohusika na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia katika kijiji cha Mbola, katika mkoa wa Tabora, Tanzania. Alitupatia maelezo kuhusu namna vijiji vya majaribio, vilivyoanzishwa barani Afrika na UM, ikijumisha kijiji cha Sauri, kiliopo Kisumu, Kenya na pia Kijiji cha Mbola, katika Tanzania.


 

 

sikiliza | hamishia mp3 | archive

Mazungumzo na Vijana wa Afrika Mashariki juu ya Masuala ya Mazingira
Kuanzia tarehe 17 mpaka 21 Juni 2008, Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP)iliandaa mkutano mkuu wa kimataifa katika mji wa Stavanger, Norway kusailia miradi ya kuhifadhi bora mazingira ulimwenguni. Mkutano ulikusanyisha wanaharakati vijana kati ya umri wa miaka 10 mpaka 14, ambao hushiriki kwenye huduma mbalimbali za kutunza mazingira katika mataifa yao. Wajumbe 700 kutoka zaidi ya mataifa 100 walihudhuria mkutano.


 

Contact us | Copyright | Terms of Service | UN home | RSS version